Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, November 18, 2012

Mapigano makali yaendelea mashariki mwa Kongo



Mapigano makali yaendelea mashariki mwa KongoMapigano makali yanaendelea kuripotiwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baina ya waasi wa M23 na vikosi vya serikali. Mashuhuda wanasema, mapigano baina ya pande mbili yanaendelea kushuhudiwa katika eneo la Kibumba lililoko jirani na mpaka wa nchi hiyo na Rwanda. Taarifa zaidi zinasema kuwa, milio ya risasi imeendelea kusikika na kuzusha wasi wasi mkubwa huku baadhi ya raia wakilazimika kuyakimbia makazi yao. Tayari Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Augustin Matata Ponyo ameutaka Umoja wa Mataifa uwawekee vikwazo viongozi wa serikali ya Rwanda kutokana na kuchochea machafuko mashariki mwa Kongo.

No comments:

Post a Comment