Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, November 29, 2012

Zaidi ya watu 30 wauawa kwenye milipuko Syria


Zaidi ya watu 30 wauawa kwenye milipuko Syria
Habari kutoka Syria zinasema kuwa milipuko kadhaa imetokea karibu na mji wa Damascus na kusababisha maafa na uharibifu mkubwa. Habari zaidi zinasema kuwa, milipuko minne ya mabomu imesikika kandokando mwa Damascus ukiwemo mji wa Jaramana yapata kilomita 10 kusini magharibi mwa Damascus. Televisheni ya Taifa ya Syria imeonyesha picha za baadhi ya maeneo yaliyokumbwa na milipuko hiyo na maafisa wa usalama wamesema uchunguzi umeanza. Baadhi ya duru zimearifu kuwa ni watu 34 waliouawa na duru zingine zimeripoti watu 40 ndio waliouawa. Serikali imeyanyooshea kidole cha lawama makundi ya wapinzani wenye silaha pamoja na mtandao wa kigaidi wa Al-qaeda ambao unawasaidia waasi hao. Mashambilizi ya mabomu mjini Damascus si jambo geni na katika miezi ya huko nyuma magenye ya watu wenye silaha yamekuwa yakitekeleza hujuma kama hizo kwa msaada wa nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani pamoja na baadhi ya nchi za Kiarabi kama vile Qatar na Saudi Arabia.

No comments:

Post a Comment