Habari kutoka Syria zinasema kuwa milipuko kadhaa 
imetokea karibu na mji wa Damascus na kusababisha maafa na uharibifu 
mkubwa. Habari zaidi zinasema kuwa, milipuko minne ya mabomu imesikika 
kandokando mwa Damascus ukiwemo mji wa Jaramana yapata kilomita 10 
kusini magharibi mwa Damascus. Televisheni ya Taifa ya Syria imeonyesha 
picha za baadhi ya maeneo yaliyokumbwa na milipuko hiyo na maafisa wa 
usalama wamesema uchunguzi umeanza. Baadhi ya duru zimearifu kuwa ni 
watu 34 waliouawa na duru zingine zimeripoti watu 40 ndio waliouawa. 
Serikali imeyanyooshea kidole cha lawama makundi ya wapinzani wenye 
silaha pamoja na mtandao wa kigaidi wa Al-qaeda ambao unawasaidia waasi 
hao. Mashambilizi ya mabomu mjini Damascus si jambo geni na katika miezi
 ya huko nyuma magenye ya watu wenye silaha yamekuwa yakitekeleza hujuma
 kama hizo kwa msaada wa nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani 
pamoja na baadhi ya nchi za Kiarabi kama vile Qatar na Saudi Arabia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment