Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, November 19, 2012

Hali ya Usalama Kenya yazidi kuwa mbaya



Hali ya Usalama Kenya yazidi kuwa mbaya
Siku moja baada ya kuuawa raia 10 kwenye shambulio la guruneti mjini Nairobi, Kenya, wanajeshi 3 wameuawa kwa kupigwa risasi leo mjini Garissa na watu wasiojulikana.
Habari zinasema kuwa wanajeshi hao walikuwa wakibadilisha gurudumu la gari lao lililokuwa limetoboka wakati watu wenye silaha walipowamiminia risasi na kuwaua. Mauaji ya hapo jana mjini Nairobi na ya leo mjini Garissa yametokea wiki moja tangu kuuawa zaidi ya maafisa 40 wa polisi katika eneo la Samburu, kaskazini mwa Kenya.
Wananchi wameelezea wasiwasi wao kuhusiana na kuzidi kudorora hali ya usalama na wameitaka serikali kuchukua hatua za dharura kuimarisha usalama haswa katika kipindi hiki ambapo nchi hiyo inajiandaa kwa uchaguzi mkuu baadaye mwaka ujao.

No comments:

Post a Comment