Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, November 3, 2012

Benki ya Dunia: Utajiri wa TZ unufaishe wananchi



Benki ya Dunia: Utajiri wa TZ unufaishe wananchi
Benki ya Dunia imesema kuwa uchumi wa Tanzania unaelekea kuimarika, lakini imeitaka serikali kuhakikisha kwamba utajiri wa nchi unawanufaisha wananchi wake ambao wengi ni masikini.  Taarifa ya benki hiyo iliyotolewa hapo jana imesema, iwapo bajeti itapangwa vyema nchini humo uzalishaji wa ndani utaongezeka kwa asilimia 6.5 hadi 7 mwaka huu, mwaka ujao na mwaka 2014, kwa kusaidiwa na uzalishaji katika sekta za madini, mawasiliano na benki. Benki ya Dunia imesema, Tanzania inaweza kufikia malengo yake iwapo itajiepusha na migogoro mikubwa ya kiuchumi na kuweka uwiano katika kukopa kwa ajili ya miradi ya miundombinu na kulipa madeni.

Aidha Benki ya Dunia imesema Tanzania ambayo ni nchi ya pili yenye uchumi unaoimarika zaidi Afrika Mashariki itaweza kupiga hatua za maendeleo kwa kasi katika miaka 7 hadi 10 ijayo kutokana na faida zitakazopatikana katika sekta ya gesi asilia. Hata hivyo Benki ya Dunia imetahadharisha kwamba umasikini mkubwa unaowakabili wananchi wengi wa Tanzania bado ni tatizo kubwa kwa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment