Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, November 15, 2012

Helkopta ya kijeshi yaanguka nchini Morocco

Helkopta ya kijeshi yaanguka nchini  Morocco Habari kutoka Guelmim kusini mwa Morocco zinasema kuwa, helikopta moja ya kijeshi imeanguka katika eneo hilo na kusababisha vifo vya wanajeshi 9. Habari zaidi zinasema wanajeshi wengine 2 wamejeruhiwa vibaya na wanaendelea kupata matibabu katika hospitali za karibu na eneo hilo. Wizara ya Ulinzi ya Morocco imesema huenda hali mbaya ya hewa ndiyo iliyosababisha ajali hiyo ingawa uchunguzi umeanzishwa kubaini chanzo chake. Mwaka uliopita takribani wanajeshi 80 walipoteza maisha yao katika eneo hilo la Guelmim  katika ajali mbaya ya ndege. Morocco ina kambi kubwa ya jeshi la wanaanga katika eneo hilo la kusini mwa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment