skip to main  |
      skip to sidebar
          
        
          
        
Waasi wa Syria wauteketeza Msikiti kwa makombora 
      
    
  
  
  
    
     
    
    
    
    
   
     Waasi wa Syria ambao wanaungwa mkono na nchi za Magharibi na hasa
 Marekani na zile za Kiarabu kama vile Saudi Arabia, Qatar na Uturuki 
wameendeleza jinai zao kwa kuushambulia kwa makombora msikiti mmoja 
ulioko katika mji wa Halab nchini humo. Picha ya mkanda wa video 
iliyotolewa hivi karibuni inawaonyesha wapiganaji hao wa kundi la waasi 
wakitenda jinai hiyo na baada ya kuuangamiza kikamilifu msikiti huo 
wakaanza kushangilia na kucheza dansi kwenye mabaki ya msikiti huo. 
Kundi hilo la waasi limefanya jinai kadhaa nchini humo ikiwa ni pamoja 
na kuwafyatulia risasi wanajeshi wa serikali baada ya kuwa 
wameshawakamata na kuwafunga kamba miguuni na mikononi. Waasi 
walianzisha machafuko nchini humo mwezi Machi 2011, kwa shabaha ya 
kuiondoa madarakani serikali halali na iliyochaguliwa na wananchi ya 
Rais Bashar Assad wa Syria.
Waasi wa Syria ambao wanaungwa mkono na nchi za Magharibi na hasa
 Marekani na zile za Kiarabu kama vile Saudi Arabia, Qatar na Uturuki 
wameendeleza jinai zao kwa kuushambulia kwa makombora msikiti mmoja 
ulioko katika mji wa Halab nchini humo. Picha ya mkanda wa video 
iliyotolewa hivi karibuni inawaonyesha wapiganaji hao wa kundi la waasi 
wakitenda jinai hiyo na baada ya kuuangamiza kikamilifu msikiti huo 
wakaanza kushangilia na kucheza dansi kwenye mabaki ya msikiti huo. 
Kundi hilo la waasi limefanya jinai kadhaa nchini humo ikiwa ni pamoja 
na kuwafyatulia risasi wanajeshi wa serikali baada ya kuwa 
wameshawakamata na kuwafunga kamba miguuni na mikononi. Waasi 
walianzisha machafuko nchini humo mwezi Machi 2011, kwa shabaha ya 
kuiondoa madarakani serikali halali na iliyochaguliwa na wananchi ya 
Rais Bashar Assad wa Syria.
    
 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
    
No comments:
Post a Comment