Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, November 26, 2012

Waasi wa Syria wauteketeza Msikiti kwa makombora



Waasi wa Syria wauteketeza Msikiti kwa makomboraWaasi wa Syria ambao wanaungwa mkono na nchi za Magharibi na hasa Marekani na zile za Kiarabu kama vile Saudi Arabia, Qatar na Uturuki wameendeleza jinai zao kwa kuushambulia kwa makombora msikiti mmoja ulioko katika mji wa Halab nchini humo. Picha ya mkanda wa video iliyotolewa hivi karibuni inawaonyesha wapiganaji hao wa kundi la waasi wakitenda jinai hiyo na baada ya kuuangamiza kikamilifu msikiti huo wakaanza kushangilia na kucheza dansi kwenye mabaki ya msikiti huo. Kundi hilo la waasi limefanya jinai kadhaa nchini humo ikiwa ni pamoja na kuwafyatulia risasi wanajeshi wa serikali baada ya kuwa wameshawakamata na kuwafunga kamba miguuni na mikononi. Waasi walianzisha machafuko nchini humo mwezi Machi 2011, kwa shabaha ya kuiondoa madarakani serikali halali na iliyochaguliwa na wananchi ya Rais Bashar Assad wa Syria.

No comments:

Post a Comment