skip to main  |
      skip to sidebar
          
        
          
        
Pillay: Waasi wa Kongo waua watoto 83 
      
    
    
     
    
    
    
    
   
     Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, makundi yanayobeba silaha 
katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yamewaua karibu watu 300 
wakiwemo watoto 83 kati ya mwezi Aprili na Septemba mwaka huu kinyume 
cha sheria katika jimbo la Kivu Kaskazini. Navanethem "Navi" Pillay Mkuu
 wa Kamisheni Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa amesema kuwa, 
makundi hayo yamefanya zaidi ya mashambulio 75 kwenye vijiji mbalimbali 
vya jimbo hilo lililogubikwa na machafuko na kuwaua watu 264 wakiwemo 
watoto 83. Pillay ameongeza kuwa, kumeshuhudiwa vitendo vya ukiukaji 
haki za binadamu na mauaji ya makumi ya wananchi wa eneo hilo katika 
miezi ya hivi karibuni. Mkuu wa Kamisheni Kuu ya Haki za Binadamu ya 
Umoja wa Mataifa ameitaka serikali ya Kongo kuchukua hatua za haraka za 
kuwalinda raia wa eneo hilo na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika 
wote ili kuzuia kuendelezwa jinai katika eneo hilo.
Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, makundi yanayobeba silaha 
katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yamewaua karibu watu 300 
wakiwemo watoto 83 kati ya mwezi Aprili na Septemba mwaka huu kinyume 
cha sheria katika jimbo la Kivu Kaskazini. Navanethem "Navi" Pillay Mkuu
 wa Kamisheni Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa amesema kuwa, 
makundi hayo yamefanya zaidi ya mashambulio 75 kwenye vijiji mbalimbali 
vya jimbo hilo lililogubikwa na machafuko na kuwaua watu 264 wakiwemo 
watoto 83. Pillay ameongeza kuwa, kumeshuhudiwa vitendo vya ukiukaji 
haki za binadamu na mauaji ya makumi ya wananchi wa eneo hilo katika 
miezi ya hivi karibuni. Mkuu wa Kamisheni Kuu ya Haki za Binadamu ya 
Umoja wa Mataifa ameitaka serikali ya Kongo kuchukua hatua za haraka za 
kuwalinda raia wa eneo hilo na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika 
wote ili kuzuia kuendelezwa jinai katika eneo hilo.
    
 
 
 
          
      
 
  
 
 
    
No comments:
Post a Comment