Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, November 15, 2012

Pillay: Waasi wa Kongo waua watoto 83


Pillay: Waasi wa Kongo waua watoto 83Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, makundi yanayobeba silaha katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yamewaua karibu watu 300 wakiwemo watoto 83 kati ya mwezi Aprili na Septemba mwaka huu kinyume cha sheria katika jimbo la Kivu Kaskazini. Navanethem "Navi" Pillay Mkuu wa Kamisheni Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa amesema kuwa, makundi hayo yamefanya zaidi ya mashambulio 75 kwenye vijiji mbalimbali vya jimbo hilo lililogubikwa na machafuko na kuwaua watu 264 wakiwemo watoto 83. Pillay ameongeza kuwa, kumeshuhudiwa vitendo vya ukiukaji haki za binadamu na mauaji ya makumi ya wananchi wa eneo hilo katika miezi ya hivi karibuni. Mkuu wa Kamisheni Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa ameitaka serikali ya Kongo kuchukua hatua za haraka za kuwalinda raia wa eneo hilo na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika wote ili kuzuia kuendelezwa jinai katika eneo hilo.

No comments:

Post a Comment