Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, December 7, 2012

'NATO na USA zaikosesha Afghanistan uthabiti'


'NATO na USA zaikosesha Afghanistan uthabiti'
Rais Hamid Karzai wa Afghanistan amekiri kwamba Shirika la Kijeshi la NATO pamoja na Marekani zinasababisha nchi hiyo ikose uthabiti. Karzai amesema, sehemu ya ukosefu usalama nchini kwake inatokana na operesheni za NATO na Marekani na kuvikosoa vikosi vya kigeni vinavyoongozwa na Marekani kwa kutekeleza mashambulizi ya usiku na kuua raia wasio na hatia
. Aidha Rais Karzai ametishia kwamba atasimamisha mazungumzo kuhusiana na hatima ya vikosi vya Marekani nchini Afghanistan. Wananchi wa Afghanistan wamezidi kukasirishwa na mauaji ya raia wasio na hatia yanayotekelezwa na vikosi vya kigeni vikiongozwa na Marekani nchini kwao. Marekani inadai kwamba inawashambulia wafuasi wa Taliban lakini raia ndio wahanga wakubwa wa mashambulizi hao.

No comments:

Post a Comment