Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, December 19, 2012

Mahakama ya ICC yamtoa hatiani Ngudjolo Chui


Mahakama ya ICC yamtoa hatiani Ngudjolo Chui
Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC imemuondoa hatiani Methieu Ngudjolo Chui kiongozi wa zamani wa kundi la wanamgambo aliyekuwa akituhumiwa kutenda jinai dhidi ya binadamu huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Mahakama ya ICC yenye makao yake mjini Hague Uholanzi ilitoa uamuzi huo hapo jana na kuamuru kuwa Ngudjolo Chui aachiwe huru mara moja. Kiongozi huyo wa zamani wa wanamgambo huko Kongo DRC alikabiliwa na tuhuma hizo baada ya kuuliwa watu mia mbili katika kijiji cha Bogoro katika mkoa wa Ituri huko mashariki mwa Kongo mwaka 2003.  Ngudjolo alikuwa akikabiliwa na makosa saba ya kutenda jinai za kivita na matatu dhidi ya binadamu.

No comments:

Post a Comment