Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, December 5, 2012

Waziri Mkuu wa Libya anusurika kuuliwa



Waziri Mkuu wa Libya anusurika kuuliwa
Kundi la watu wenye silaha waliokuwa na lengo la kumuua Waziri Mkuu wa Libya Ali Zaidan jana walilishambulia gari la Waziri Mkuu huyo katika mji wa al Baida umbali wa kilomita 200 kutoka mji wa Benghazi hata hivyo alinusurika kifo. Ali Zaidan alikutwa na mashambulizi hayo akiwa njiani kuelekea katika mji wa al Baida kwa ajili ya kufanya mazungumzo na viongozi wa mji huo.
Hata hivyo magari yaliyokuwa yakifuatana na Waziri Mkuu wa Libya yameharibiwa vibaya katika mashambulizi hayo. Baadhi ya maeneo ya Libya hadi sasa yangali yanashuhudia mapigano ambapo serikali mpya ya nchi hiyo imeamua kuchukua hatua kali za kupambana na makundi hayo yenye silaha ambayo yanamiliki silaha kinyume cha sheria.

No comments:

Post a Comment