Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, December 29, 2012

22 wafa katika ajali ya jahazi Guinea Bissau


22 wafa katika ajali ya jahazi Guinea Bissau
Watu wasiopungua 22 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 70 hawajulikani waliko baada ya jahazi waliyopanda kuzama nchini Guinea Bissau. Taarifa zinasema kuwa, jahazi hilo lilizama huku ikiwa imebeba zaidi ya abiria 97 ikitoka katika kisiwa cha Boloma kilichopo katika bahari ya Atlantiki na kuelekea bandari ya Bissau magharibi mwa Afrika. Duru za hospitali zinasema kuwa, hadi sasa viwiliwili vya wahanga 22 vimehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti, huku juhudi zikiendelea za kuwatafuta wahanga wengine 72 ambao hawajulikani waliko. Chanzo cha ajali hiyo imeelezwa kuwa ni kupakia abiria kupita kiasi na shehena kubwa ya mizigo.

No comments:

Post a Comment