Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, December 4, 2012

Sudan yasisitiza kujibu uchokozi wa Israel


Sudan yasisitiza kujibu uchokozi wa Israel
Waziri wa Habari na Utamaduni wa Sudan amesisitiza kwamba, Khartoum ina haki ya kutoa jibu kwa hujuma na uchokozi wa Israel. Ahmed Bilal Othman amesema, kwa mtazamo wa Khartoum ni kuwa faili la hujuma, uchokozi na shambulio la Israel dhidi ya Sudan bado liko wazi na kwamba, muda ukiwadia nchi hiyo itatoa jibu kwa uchokozi huo. Amesema, nchi hiyo inaendelea kukusanya nyara na ushahidi kuhusu shambulio la kichokozi la Israel dhidi ya Sudan ili kuwasilisha ushahidi huo kwa asasi za kieneo na kimataifa likiwemo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Itakumbukwa kuwa Oktoba 24 mwaka huu, ndege nne za kivita za Israel zilishambulia kiwanda cha kutengeneza silaha cha Yarmouk huko Sudan.

No comments:

Post a Comment