Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, December 20, 2012

Somalia tayari kuwafungulia mashtaka maharamia


Somalia tayari kuwafungulia mashtaka maharamiaMkuu wa Mahakakama ya Juu ya Somalia Aydiid Abdullahi IIka Hanaf amesema maharamia Wasomali waliokamatwa katika maji ya kimataifa watafunguliwa mashtaka ndani ya Somalia.
Katika mahojiano na tovuti ya Shabelle, IIka Hanaf amesema mfumo wa sheria wa Somalia sasa una uwezo wa kuwafungulia mashtaka maharamia na kwamba hakuna haja ya wahalifu hao kufikishwa katika mahakama za nchi za kigeni.
Katika miaka ya hivi karibuni, maharamia Wasomali wamekuwa wakikamatwa katika eneo la Bahari ya Hindi na kufunguliwa mashtaka katika nchi za Ulaya, Asia, Afrika na hata Marekani. Maharamia wakiwa na silaha nzito nzito huteka nyara meli na kuziachilia baada ya kupokea mamilioni ya dola kama kikomboleo.

No comments:

Post a Comment