Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, December 21, 2012

Viongozi wa kidini nchini Misri waandamana


Viongozi wa kidini nchini Misri waandamana
Viongozi wa kidini nchini Misri wamefanya maandamano ya kulaani hatua ya wafuasi wa rais wa zamani wa nchi hiyo, dikteta Hosni Mubarak, ya kufanya mashambulizi dhidi ya viongozi hao na misikiti nchini humo. Duru za habari zimeunukuu muungano wa viongozi hao ukisema kwamba, leo wamefanya maandamano hayo mbele ya msikiti wa "Ibrahim" katika mji wa Alexandria kaskazini mwa Misri. Wamesema kuwa, wafuasi wa utawala wa kidikteta wa Hosni Mubarak kwa kushirikiana na makundi yanayochukia dini ya kisekula na kileberali, wamekuwa wakiwashambulia viongozi wa kidini na kuwazuia kuadhini na kuqimu sala katika baadhi ya misikiti,
suala ambalo wanasema halijawahi kushuhudiwa katika historia ya Misri. Ripoti hiyo imeeleza kuwa, lengo la vitendo hivyo dhidi ya Uislamu vinavyofanywa na wafuasi wa dikteta Hosni Mubarak na makundi ya kisekula na kileberali, ni kuzusha fitina kati ya wafuasi wa dini mbalimbali nchini humo, suala ambalo wamesema, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Misri inatakiwa kukabiliana nalo vilivyo. Muungano huo umesisitiza kuwa, shambulizi la hivi karibuni dhidi ya Sheikh Ahmad al-Mahlawi na Waislamu wapatao 150, wa msikiti wa Ibrahim mjini Alexandria ni ushahidi tosha wa kushadidi vitendo hivyo.

No comments:

Post a Comment