Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, December 24, 2012

Mpatanishi wa mgogoro wa Syria akutana na Assad


Mpatanishi wa mgogoro wa Syria akutana na  Assad
Lakhdar Brahimi mwakilishi wa Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu katika mgogoro wa Syria amekutana na Rais Bashar al Assad mjini Damascus na kujadili mgogoro wa nchi hiyo.
Brahimi amesema pande hizo mbili zimebadilishana mawazo na kuchunguza njia gani zichukuliwe kwa ajili ya mustakbali wa nchi hiyo.
Katika upande mwingine Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amekosoa uungaji mkono wa nchi za Magharibi kwa magaidi wa Syria na kusema kwamba jambo hilo halikubaliki kabisa. Sergei Lavrov amesema, uungaji mkono wa nchi za Magharibi kwa magaidi wa Syria kwa kisingizo kuwa ni magaidi wazuri, ni jambo lisilokubalika. Ameongeza kuwa, iwapo pande za Magharibi zitaanza kuyagawa makundi ya kigaidi kati ya magaidi wabaya na magaidi wanaokubalika, suala hilo litahatarisha usalama wa Mashariki ya Kati na dunia nzima kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment