Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, December 30, 2012

Mkutano wa al Bashir na Kiir kufanyika Januari 13


Rais Omar al Bashir wa Sudan (kushoto) na Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini
Rais Omar al Bashir wa Sudan (kushoto) na Rais Salva Kiir wa Sudan KusiniEthiopia imeainisha tarehe 13 Januari kuwa siku ya kufanyika mkutano kati ya Marais wa Sudan na Sudan Kusini Omar al Bashir na Salva Kiir huko Addis Ababa mji mkuu uwa Ethiopia. Hailemariam Dessalegn, Waziri Mkuu wa Ethiopia amewataka marais hao wawili kuhudhuria mkutano huo kama ilivyopangwa. Wiki iliyopita Waziri Mkuu wa Ethiopia alizitembelea Khartoum na Juba na kuhakikishiwa kwamba Marais hao wa Sudan mbili watashiriki kwenye mkutano huo. Mkutano ujao kati ya Rais Omar al Bashir wa Sudan na mwenzake wa Sudan Kusini,
Salva Kiir utajaribu kutafuta njia za kufanikisha makubaliano ya pamoja ya ushirikiano yaliyosainiwa na nchi mbili hizo mwezi Septemba mwaka huu huko Addis Ababa sambamba na kutatua pia masuala yaliyokwamisha utekelezaji wa makubaliano hayo.  Waziri Mkuu wa Ethiopiai amesema kuwa, ziara yake ya hivi karibuni huko Khartoum ilikuwa na lengo la kuimarisha uhusiano uliasisiwa na hayati Meles Zenawi, Waziri Mkuu wa zamani wa Ethiopia.

No comments:

Post a Comment