Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, December 19, 2012

Mubarak atakiwa kuhamishiwa jela ya kijeshi Misri


Mubarak atakiwa kuhamishiwa jela ya kijeshi Misri
Idara ya jela za Misri iliyo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi hiyo imetaka Hosni Mubarak, dikteta wa zamani wa nchi hiyo ahamishiwe katika jela ya kijeshi ya al Maadi. Idara ya jela za Misri imeiomba Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo kuafiki suala la kumhamishia Hosni Mubarak katika hospitali ya kijeshi iliyo karibu na jela hiyo kwa kuzingatia hali mbaya aliyonayo katika chumba maalumu anakoshikiliwa huko katika hospitali ya  jela ya Tura, kusini mwa Cairo. Muhammad Ibrahim Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Misri ambaye pia ni mkuu wa idara ya jela za Misri ameeleza kuwa hali ya Hosni Mubaraka ni mbaya na kwamba anapasa kulazwa hospitalini.
Siku tatu zilizopita Hosni Mubarak alianguka chini huko katika hospitali ya Tura na kujeruhiwa sehemu za kichwani. 

No comments:

Post a Comment