Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, December 17, 2012

Chama cha Chavez chashinda uchaguzi wa kieneo


Chama cha Chavez chashinda uchaguzi wa kieneo
Chama cha kisoshalisti cha Rais Hugo Chavez wa Venezuela kimeshinda katika uchaguzi wa kieneo nchini humo.
Matokeo yanaonesha kuwa, wafuasi wa Chavez wameshinda ugavana katika majimbo 20 kati ya 23 kwenye uchaguzi uliofanyika Jumapili.
 Hii ni katika hali ambayo nchi hiyo bado inashughulishwa na hali ya kiafya ya Chavez ambaye amepata nafuu baada ya kufanyiwa operation hivi karibuni huko Cuba. Huo ulikuwa upasuaji wa 4 kufanyiwa kiongozi huyo tangu ilipojulikana kuwa ana ugonjwa wa saratani mwaka 2011.
Chavez anatarajiwa kuanza kipindi chake kipya cha urais Januri 10. Lakini iwapo atashindwa kuongoza nchi kutoakana na hali yake ya kiafya itabidi uchaguzi mpya wa rais ufanyike katika kipindi cha siku 30.

No comments:

Post a Comment