Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, December 24, 2012

Watoto 11 wafariki dunia katika ajali ya gari huko China


Watoto 11 wafariki dunia katika ajali ya gari huko China
Watoto 11 wa shule wamefariki dunia baada ya basi dogo lililokuwa limebeba abiria wengi kutumbukia kwenye dimbwi huko katika mkoa wa Jiangxi nchini China.
Basi hilo lililokuwa na watu 17 asubuhi ya leo kwa wakati wa China lilitumbukia katika dimbwi lililokuwa kando ya barabara karibu na mji wa Guixi. Maafisa wa eneo hilo wameripoti kuwa watu sita wakiwemo wanafunzi wanne, mwalimu na dereva wameondolewa kutoka sehemu ya ajali hiyo  na kupelekwa hospitalini.
Wahanga wa ajali hiyo walikuwa watoto waliokuwa na umri wa kati ya miaka minne na sita. Polisi ya China imemlaumu dereva kwa ajali hiyo na imefanikiwa kumtia mbaroni masaa machache baada ya ajali hiyo. Itakumbukwa kuwa baadhi ya barabara za China ni miongoni mwa barabara hatari duniani zinazosababisha makumi ya maelfu ya vifo vya watu kila mwaka.

No comments:

Post a Comment