Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, December 30, 2012

Marekani yazidi kujizatiti kijeshi barani Afrika


Wanajeshi wa Chad wakipiga doria katika mji mkuu N'djamena
Wanajeshi wa Chad wakipiga doria katika mji mkuu N'djamena
Marekani imetuma vikosi vyake nchini Chad katika hatua ambayo inaonekana wazi ni kuzidi kujizatiti kijeshi barani Afrika.
Sababu iliyotajwa na Marekani ya kutuma vikosi vyake nchini Chad ni wasiwasi wa Washington kuhusu usalama wa raia wake kutokana na kuzidi kusonga mbele waasi katika nchi jirani na Chad yaani Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Katika barua yake kwa maspika wa mabunge mawili ya Marekani, Rais Barack Obama wa nchi hiyo amesema kuwa, raia kadhaa wa Marekani wameondolewa katika mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Bangui tangu tarehe 27 Disemba na hivi sasa kikosi cha wanajeshi 50 wa Marekani kimetumwa nchini Chad.

Watu wanaokosoa hatua hiyo ya Marekani wanasema kuwa, hawaoni sababu ya Washington kutuma kikosi kizima cha jeshi tena katika nchi ambayo haina machafuko kwa madai kuwa nchi jirani ina machafuko hasa kwa vile tayari Marekani na Ufaransa zimekataa mwito wa Rais Francois Bozize wa Jamhuri ya Afrika ya Kati wa kusaidiwa kukabiliana na waasi wa kundi la SELEKA.

No comments:

Post a Comment