Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, December 5, 2012

Serikali na waasi wa Kongo kufanya mazungumzo



Serikali na waasi wa Kongo kufanya mazungumzo
Mazungumzo kati ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na waasi wa mashariki mwa nchi hiyo yanatazamiwa kufanyika wiki hii. Hayo yamesemwa na maafisa wa nchi jirani na Kongo baada wa waasi wa M23 kuondoka katika mji wa Goma. Maafisa wawili wa Uganda ambao wamekuwa wakijaribu kufanikisha  mazungumzo kati ya serikali ya Kinshasa na waasi wa M23 wamesema kuwa pande mbili hizo zinatarajia kukutana Kampala Uganda wiki hii. Afisa wa ngazi ya juu wa Kinshasa pia ameeleza kuwa ujumbe wa Kongo unaowajumuisha wabunge na waziri mmoja unatazamiwa kuwasili Kampala wiki hii kwa ajili ya mazungumzo hayo.


No comments:

Post a Comment