Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, December 9, 2012

Wananchi wa Mali waunga mkono uingiliaji wa kijeshi



Wananchi wa Mali waunga mkono uingiliaji wa kijeshi Raia kadhaa wa Mali wameandamana huko Bamako mji mkuu wa nchi hiyo wakiitaka jamii ya kimataifa iingilie kijeshi mgogoro wa kaskazini mwa nchi hiyo. Wafanya maandamano wametaka uingiliaji kijeshi wa haraka huko kaskazini mwa Mali kwa ajili ya kuyakomboa maeneo yanayoshikiliwa na makundi ya waasi yanayodaiwa kuwa na uhusiano na mtandao wa al Qaida.
Vijana wengi wa Mali wametangaza kuwa wako tayari kujiunga jeshini ili kushiriki kwenye oparesheni za kukomboa maeneo ya kaskazini mwa nchi hiyo. Baada ya wanajeshi wa Mali kufanya mapinduzi tarehe 22 Machi mwaka huu makundi ya kabila la Tuareg na Ansaruddin tawi la mtandao wa al Qaida  yalidhibti eneo la kaskazini mwa nchi hiyo na hadi sasa maeneo mengi ya kihisoria na kidini yameharibiwa na kubomolewa na makundi hayo yenye misimamo mikali huku raia wa maeneo hayo wakilazimika kuyakimbia makazi yao.

No comments:

Post a Comment