Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, December 10, 2012

Rais Kikwete awataka Watanzania kudumisha amani


Rais Kikwete awataka Watanzania kudumisha amani
Rais Jakaya Kikwete wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewataka watanzania kudumisha, amani, usalama na umoja. Rais Kikwete amesema hayo wakati wa maadhimisho ya miaka 51 ya uhuru wa Tanganyika yaliyofanyika hapo jana na kuonyesha kukerwa na watu wanaobeza maendeleo ya Tanzania. Rais Kikwete amesema, wenye hila na chuki ndio wanaobeza maendeleo ya Tanzania. Rais Kikwete aliyeongoza sherehe za uhuru wa Tanzania Bara katika uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam amesema, nchi hiyo inatimiza miaka hiyo ikiwa na amani, umoja na utulivu, lakini pia ikiwa imefanya vizuri katika upande wa maendeleo ya kiuchumi. Aidha Rais Kikwete alizitumia sherehe za maadhimisho ya miaka 51 ya uhuru wa Tanganyika kutoa msamaha kwa wafungwa zaidi ya 3000 na kutoa Nishani ya Uhuru kwa watu mbalimbali wakiwemo wanasiasa na wasanii.    

No comments:

Post a Comment