Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, December 11, 2012

Wamisri: tutafuata njia ya Mapinduzi ya Kiislamu



Wamisri: tutafuata njia ya Mapinduzi ya Kiislamu  Katibu Mkuu wa Chama cha Kiislamu cha Misri ametangaza kuwa Wamisri wanataka kufuata njia ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran.
Majid Ahmad Hussein Katibu Mkuu wa Chama cha Kiislamu cha Misri amesema kuwa wananchi wa nchi hiyo wanataka kufuata njia ya Mapinduzi ya Kiislamu na kuongeza kuwa Mashariki ya Kati ni eneo muhimu ulimwenguni  na kwamba Marekani inataka kumshinikiza Rais Mursi wa Misri asiwasaidie Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza na aupatie utawala wa Kizayuni gesi pamoja na kuudhaminia usalama.

Mwanasiasa huyo wa Misri ameendelea kusema kuwa adui mkubwa wa mwamko wa Kiislamu si madikteta na wala vibaraka wao, bali ni Marekani na Utawala wa Kizayuni.

No comments:

Post a Comment