
amani na uthabiti umerejea baada ya kukombolewa mji wa Jowhar na wanamgambo wengi wa kundi hilo wameukimbia mji huo. Wakati huohuo, mawaziri watatu wa serikali ya Somalia wamenusurika kifo baada ya kushambuliwa na wanamgambo wa al Shabab kwenye mji wa Merca ulioko umbali wa kilomita 100 kusini mwa Mogadishu. Inafaa kuashiria hapa kuwa, hapo jana vikosi vya serikali ya Somalia vilifanikiwa kuwauwa waasi 27 wa kundi la al Shabab na kuwajeruhi wengine 40 baada ya kutokea mapigano makali katika mji wa Bardera ulioko kusini mwa mkoa wa Gedo.
No comments:
Post a Comment