Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, December 13, 2012

Waziri wa Ulinzi wa Misri ataka mazungumzo ya kitaifa


Waziri wa Ulinzi wa Misri ataka mazungumzo ya kitaifa
Waziri wa Ulinzi wa Misri ameyaalika makundi yote kushiriki katika mkutano uliopangwa kufanyika leo huko Cairo mji mkuu wa nchi hiyo. Meja Jenerali Abdulfatah al Sisi ambaye pia ni Mkuu wa vikosi vya majeshi ya Misri ameeleza kuwa mkutano huo wa leo hautazungumzia kuhusu siasa wala kura ya maoni ya katiba bali watakaa pamoja kama Wamisri.
Kamati ya kisheria inayosimamia kura ya maoni imeamua kwamba kura hiyo ya maoni inapasa kufanyika kwa muda wa siku mbili badala ya siku moja.  Kamati hiyo ilimuomba rasmi Rais Muhammad Mursi kuwasilisha sheria inayoidhinisha kuwa kura ya maoni ifanyike katika awamu mbili yaani Jumamosi ya tarehe 15 na Jumamosi ya tarehe 22 mwezi huu. Mapema jana raia wa Misri wanaompinga Rais wa nchi hiyo walivuka vizuizi vilivyokuwa vimewekwa kwa ajili ya kuilinda ikulu ya Rais huyo katika kuonyesha upinzani wao kwa rasimu ya katiba iliyowasilishwa hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment