Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, December 30, 2012

Jinai za utawala wa Aal Khalifa hazitaendelea milele

Jinai za utawala wa Aal Khalifa hazitaendelea milele
Mkuu wa Kamati ya Kupambana na Mateso nchini Bahrain ameeeleza kuwa vitendo vya mabavu vya utawala wa kifalme wa ukoo wa Aal Khalifa na kuwakandamiza raia wa nchi hiyo vimebadilika na kuwa siasa za kila siku za utawala huo na kwamba bilaya  shaka yoyote siasa  hizo haziwezi kudumu milele.
Rodney Shakespeare, Mkuu wa Kamati ya Kupambana na Mateso nchini Bahrain amemtaja Waziri Mkuu wa Bahrain ambaye kwa zaidi ya miaka 40 iliyopita anashikilia wadhifa huo kuwa ndiye mhusika mkuu wa kuuliwa watoto, kutiwa mbaroni wanawake na kuteswa wafungwa huko Bahrain.
Amesisitiza kuwa utawala wa Bahrain hauna mpango wa kuendesha uchaguzi wowote nchini humo kwa sababu kufanyika uchaguzi wa aina yoyote nchini humo kutakuwa sawa na kuuondoa madarakani utawala wa ukoo wa Aal Khalifa.  Shakespeare amesisitiza namna utawala wa Manama unavyopinga demokrasia na kueleza kuwa utawala wa Aal Khalifa hatimaye utasalimu  amri  tu mbele ya matakwa ya wananchi.  Harakati za mapinduzi za wananchi wa Bahrain zilianza Februari 14 mwaka jana na  hadi sasa mamia ya raia wameuliwa, kujeruhiwa na kutiwa nguvuni kufuatia mashambulizi ya vikosi vya Bahrain vikishirikiana na vikosi vamizi vya Saudi Arabia dhidi ya raia wanaoandamana.

No comments:

Post a Comment