Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, December 31, 2012

Migodi 4000 ya dhahabu yagunduliwa Darfur


Migodi 4000 ya dhahabu yagunduliwa Darfur Waziri wa Madini wa Sudan ametangaza habari ya kugunduliwa migodi 4000 ya dhahabu huko Jebel Amir katika jimbo la Darfur ya Kaskazini yenye uwezo wa kuzalisha tani 15 za dhahabu kwa mwaka sawa na kilo 70 kwa siku. Kamal Abdullatif amewaambia waandishi wa habari baada ya mkutano wa baraza la mashauriano la Wizara ya Madini ya Sudan kwamba wizara yake itaendelea kuzalisha madini hayo ili kuboresha uchumi wa taifa.

Waziri wa Madini wa Sudan amesema kuwa mwaka jana uuzaji wa dhahabu ulichangia pato la dola bilioni mbili la taifa na makampuni yanayoendesha shughuli zake katika machimbo ya dhahabu yanatazamiwa kufikia 15 hadi mwakani.
Kamal Abdullatif ameutaja uzalishaji wa dhahabu huko Jebel Amir kuwa usio na kifani kwa kuwa vijana wengi wameacha na harakati za uasi na kujishughulisha na uchimbaji madini.

No comments:

Post a Comment