Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, December 7, 2012

Maandamano ya kupinga kushambuliwa Mashia



Maandamano ya kupinga kushambuliwa Mashia Maandamano makubwa yanatarajiwa kufanyika hii leo mjini New York Marekani kupinga kuongezeka mashambulizi dhidi ya Waislamu wa Kishia katika nchi mbalimbali duniani.
Kundi la Kongresi ya Waislamu ambalo ni taasisi ya kitamaduni ya Waislamu wa Kishia nchini Marekani ndiyo imetisha maandamano hayo yatakayofanyika leo mjini New York.
Taasisi hiyo imesema katika taarifa yake kwamba, Waislamu wa Amerika Kaskazini watashiriki katika maandamano hayo kwa lengo la kupinga na kuzuia kushtadi mashambulio dhidi ya Waislamu wa Kishia katika nchi za Pakistan, Afghanistan, Iraq, Saudi Arabia, Syria na Yemen.  Taarifa hiyo imesisitiza kwamba, katika wiki mbili zilizopita mamia ya Waislamu wa Kishia wameuawa kwenye nchi hizo. 

No comments:

Post a Comment