Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, December 29, 2012

Waasi wa J/A/Kati wakubali kuzungumza na serikali



Waasi wa J/A/Kati wakubali kuzungumza na serikali
Wawakilishi wa serikali ya Jamhuri ya Afrika ya Kati na waasi wa Seleka wameafikiana juu ya kufanya mazungumzo ya amani. Guy - Pierre Garcia Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Uchumi ya Nchi za Afrika ya Kati amesema kuwa, wawakilishi wa  serikali ya Bangui na waasi wa Seleka hapo jana walikubaliana  kuanza  kufanya mazungumzo bila ya masharti. Baadhi ya duru zinasema kuwa, mazungumzo kati ya pande hizo mbili yenye lengo la kuleta amani na uthabiti nchini humo yatafanyika tarehe 10 Januari mwakani huko Libreville, mji mkuu wa Gabon. Waasi wa Seleka walianzisha operesheni kamambe ya kijeshi wiki mbili zilizopita, na sambamba na kuteka miji kadhaa walikuwa wanaukaribia mji mkuu wa nchi hiyo Bangui.

No comments:

Post a Comment