Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, December 30, 2012

UN yahuzunishwa na kifo cha aliyebakwa India


UN yahuzunishwa na kifo cha aliyebakwa IndiaKatibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameeleza kusikitishwa na kifo cha mwanachuo wa kike aliyekuwa akisomea taaluma ya udaktari huko India, aliyefariki dunia baada ya kubakwa na wanaume sita ndani ya basi la abiria lililokuwa katika mwendo.  Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, Ban Ki Moon amesikitishwa na kifo cha msichana huyo wa Kihindi na kutoa mkono wa pole kwa familia na ndugu wa mhanga wa jinai hiyo. Ban Ki moon pia ameitaka serikali ya India kuchukua hatua kali ili kuzuia kukaririwa tena janga kama hilo huko India. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametaka kupewa adhabu kali waliotenda jinai hiyo na kuwasaidia waathiriwa wengine wa jinai kama hiyo huko India. Msichana huyo wa Kihindi aliyekuwa na umri wa miaka 23 alivamiwa na kubakwa na wanaume sita tarehe 16 mwezi huu na aliaga dunia jana akiwa hospitalini kwa matibabu nchini Singapore.

No comments:

Post a Comment