Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, December 29, 2012

Utawala wa Bahrain wafananishwa na Wanazi


Utawala wa Bahrain wafananishwa na WanaziMkuu wa Kamati ya Kupambana na Vitendo vya Utesaji nchini Bahrain ameufananisha utawala wa Aal Khalifa wa nchi hiyo na utawala wa Wanazi nchini Ujerumani  na kuongeza kuwa, Waziri Mkuu wa Bahrain ni mtuhumiwa nambari moja katika kuwauwa wanawake na kuwatesa wananchi wa nchi hiyo. Amesema kuwa utawala wa Aal Khalifa hauthubutu hata mara moja kuitisha uchaguzi huru nchini Bahrain, kwani unajua wazi kwamba uchaguzi wowote utakaofanyika nchini humo utaung'oa utawala huo wa kifalme. Ameongeza kuwa, Waziri Mkuu wa Bahrain ni mtenda jinai nambari moja katika kuwauwa watoto,
wanawake, kuwafyatulia risasi waandamanaji mjini Manama na kuwatia mbaroni wananchi na hatimaye kuwatesa wakiwa korokoroni au gerezani. Mkuu wa Kamati ya Kupambana na Vitendo vya Utesaji nchini Bahrain amezihutubu nchi za Magharibi  kwa kusema kwamba, nchi hizo lazima zielewe kwamba utawala wa Aal Khalifa kwa kushirikiana na utawala wa Aal Saud wa Saudi Arabia zinakandamiza demokrasia nchini humo. Amezituhumu pia tawala hizo kwa kuyasaidia makundi ya kigaidi nchini Syria na hata zinaandaa mazingira kwa waasi wa Syria kutumia silaha za kemikali nchini humo.

No comments:

Post a Comment