Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, December 10, 2012

M23: Serikali ndio chanzo cha mapigano mashariki


M23: Serikali ndio chanzo cha mapigano masharikiWaasi wa M23 walioanza mazungumzo yao jana katika mji mkuu wa Uganda Kampala wameituhumu serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwamba, ndio chanzo cha machafuko mashariki mwa nchi. Francois Tuyihimbaze Katibu Mkuu wa M23 na mkuu wa timu ya mazungumzo ya waasi hao ameikosoa vikali serikali ya Kinshasa.
Akizungumza katika kikao baina ya timu yao na serikali huko Kampala, afisa huyo mwandamizi wa M23 amesisitiza kuwa, uongozi mbaya ndicho chanzo kikuu cha kutokea mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kufuatia tuhuma hizo ujumbe wa Kinshasa katika mazungumzo hayo umetishia kujitoa katika mazungumzo hayo. Waziri wa Ulinzi wa Uganda Crispus Kiyonga amethibitisha kujitokeza tofauti na mivutano hiyo hata hivyo amesisitiza kwamba, kuanza kwa mazungumzo hayo kumehuisha matumaini ya kupatikana suluhu baina ya pande mbili.

No comments:

Post a Comment