Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, December 21, 2012

Makumi ya waasi wajisalimisha kwa serikali Sudan


Makumi ya waasi wajisalimisha kwa serikali SudanMakumi ya waasi wamejisalimisha kwa jeshi la Sudan. Mtandao wa habari wa Sudan Safari umeeleza kuwa, karibu viongozi 22 wa kundi la waasi la "Mrengo wa Mapinduzi" na makundi mengine ya waasi ambayo yanaendesha shughuli zao katika eneo la Abyei, wameamua kuweka chini silaha zao na kujisalimisha kwa askari wa serikali. Rahmat Abdur-Rahman, mmoja wa viongozi wa eneo la Abyei huko kusini mwa Sudan, amenukuliwa akisema kuwa, viongozi hao wa waasi wamethibitisha kuwa, makundi ya waasi hivi sasa yamedhoofika na yanazidi kupoteza nguvu zao siku hadi siku. Kwa mujibu wa viongozi hao wa waasi,
wafuasi wengi wa makundi ya waasi wanataraji kujisalimisha hapo baadaye. Abyei ni eneo la kusini mwa Sudan lenye utajiri mkubwa wa mafuta, ingawa Sudan Kusini inadai ni mali yake na inawasaidia waasi kupigana na serikali ya Sudan na kila anayeiunga mkono serikali ya Khartoum.

No comments:

Post a Comment