Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, December 4, 2012

Watu 10 wauawa katika jimbo la Borno Nigeria



Watu 10 wauawa katika jimbo la Borno Nigeria Kwa uchache watu 10 wameuawa baada ya watu wanaobeba silaha kushambulia Kanisa moja lililoko katika kijiji cha Chibok  kilichopo katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria. Kwa upande mwengine, askari polisi wawili wameuawa kwenye shambulizi lililofanywa na kundi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Shambulio hilo limefanyika katika eneo la Maiduguri lililoko umbali wa kilomita 140 kutoka jimbo la Borno.
Taarifa zinasema kuwa, waasi hao wa Boko Haram waliteketeza moto kituo kimoja cha polisi kilichoko katika mji wa Gamboru Ngala jimboni humo. Hadi sasa mamia ya watu wameshapoteza maisha yao na majengo kadhaa ya serikali  na Makanisa kuchomwa moto kutokana na mashambulio yanayofanywa na kundi la Boko Haram kaskazini mwa Nigeria

No comments:

Post a Comment