skip to main |
skip to sidebar
Padri Ambros Mkenda apigwa risasi Zanzibar
Watu wasiojulikana wamempiga risasi Padri Ambros Mkenda wa Kanisa
Katoliki la Mpendae mjini Zanzibar na kumjeruhi. Kamanda wa Polisi wa
Mkoa wa Mjini Magharibi Aziz Juma Muhammed amethibitisha tukio hilo huku
jeshi la polisi likiendelea kuchunguza ili kubaini wahusika wa uhalifu
huo. Askofu Michael Hafidh wa Kanisa la Anglikan la Mkunazini alidai
hivi karibuni kumekuwepo vipeperushi vilivyosambazwa vikiwatisha watu
wenye imani ya Kikristo na kuiomba serikali iongeze ulinzi na kuimarisha
usalama. Aidha ameiomba serikali kuchukua hatua za tahadhari kwani
matukio kama hayo yameanza kutokea kwa viongozi wa dini kuanzia kwa
Sheikh Soraga aliyemwagiwa tindikali na hivi sasa Padri Ambros.
Hata
hivyo Kamanda Aziz Muhammed amekanusha madai hayo na kusema kuwa
wanalichukulia tukio hilo kuwa la kawaida tu la kihalifu na pia kuongeza
hawana vipeperushi vya aina yoyote vinavyoelezea kutishwa viongozi wa
kidini wala hawaamini kwamba matukio hayo yanafanywa dhidi ya dini
fulani. Ameongeza kuwa, Padri Ambros ni mhasibu kanisani na kwamba
huenda hiyo ndiyo sababu iliyopelekea kushambuliwa na wahalifu
waliodhani kuwa amebeba pesa.
No comments:
Post a Comment