Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, December 26, 2012

Marekani katika magendo ya silaha Afrika


Marekani katika magendo ya silaha Afrika
Nchi zilizoko katika eneo la kusini mwa Sahara Kuu huko kaskazini mwa Afrika, zimegeuka kuwa moja kati ya masoko muhimu ya magendo ya silaha ulimwenguni katika kipindi cha miongo ya hivi karibuni. Duru zinasema kuwa, Marekani imekuwa kinara katika kulibadilisha eneo hilo kuwa soko kuu la magendo ya silaha duniani. Duru hizo zimeeleza kuwa, nchi za China na Russia nazo pia zimetumbukia kwenye mkumbo huo kwani zinatoa mikopo kama inavyofanya Marekani kwa minajili ya kuuza silaha zao katika eneo hilo. Silaha zinazouzwa kwa magendo katika eneo hilo la Sahara Kuu zinaangukia mikononi mwa maeneo yanayokumbwa na mapigano ya kikabila, na maeneo ambayo yanadhibitiwa na waasi kama vile Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Somalia. Taarifa zinasema kuwa, silaha hizo licha ya kuchangia machafuko, huongeza hatari ya kuibuka mapigano mapya ya ndani na nje ya mipaka ya nchi hizo.

No comments:

Post a Comment