Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, December 17, 2012

Sudan yakaribisha AU kutatua mzozo wa Abyei


 Sudan yakaribisha AU  kutatua mzozo wa Abyei
Chama tawala cha Sudan cha Kongresi ya Taifa kimekaribisha uamuzi wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika wa kubuni mpango kwa ajili ya kutatua mgogoro wa Abyei katika kikao chake kijacho.
Chama hicho kupitia mwenyekiti wake Adam Yusuph ambaye ni Makamu wa Rais wa Sudan sambamba na kusifu nafasi ya AU katika kutatua migogoro ya kieneo, kimesema kuwa kadhia ya Abyei inapaswa kujadiliwa kwenye kikao hicho cha AU kilichopangwa kufanyika mwezi Januari. Chama hicho pia kimesisitiza kwamba, viongozi wa Kiafrika wanapaswa kuutafutia mgogoro wa Abyei suluhisho litakalokubaliwa na pande zote mbili.
Eneo lenye utajiri wa mafuta la Abyei lililoko kusini mwa Sudan lilitakiwa kupigia kura ya maoni Januri mwaka huu ili kuainisha hatima yake lakini hitilafu za Sudan na Sudan Kusini juu ya watu wanaopaswa kushiriki kura hiyo zimesababisha zoezi hilo liakhirishwe.

No comments:

Post a Comment