Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, December 2, 2012

WANAJESHI WANNE MBEYA WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KOSA LA MAUAJI

 KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA DIWANI ATHUMANI

Na, Gordon Kalulunga, Mbeya

JESHI la polisi mkoani Mbeya limewafikisha mahakamani askari wa Nne wa Jeshi la wananchi wa Tanzania kwa tuhuma za mauaji.

Taarifa ya Jeshi la Polisi mkoani Mbeya iliyosainiwa na Kamanda wa polisi wa mkoa huo Diwani Athumani iliyotumwa kwa vyombo vya habari jana, imesema kuwa mnamo Novemba 18 huko katika hospitali teule ya wilaya ya Mbeya Vijijini Petro Sanga (25) alifariki dunia akipatiwa matibabu baada ya kuchomwa kisu.

Kamanda Diwani Athumani kupitia taarifa hiyo amesema kuwa marehemu alichomwa kisu shingoni na kikundi cha watu wanaosadikiwa kuwa ni wanajeshi kikosi cha 44 KJ Mbalizi akiwa kwenye Grocery inayoitwa Vavene Mwe.

‘’Marehemu baada ya watu hao kuvamia Bar iitwayo Power Night Club na kuwapiga ambamo awali alikuwepo na kushambuliwa alijaribu kukimbia toka eneo hilo hadi katika Grocery hiyo lakini watu hao walimkimbiza hadi eneo la hilo na kumjeruhi vibaya kwa kumchoma kisu.

Amesema chanzo cha tukio hil ilikuwa ni kulipiza kisasi baada ya askari Godfrey Matete(30) wa kikosi hicho kupigwa na walinzi wa kilabu cha pombe za kienyeji kiitwacho DDC  kilichopo Mbalizi ambapo askari huyo alifungua kesi katika kituo cha polsi cha Mbalizi ambapo walinzi hao wane walikamatwa.

Amewataja walinzi ambao walikamatwa kuwa ni pamoja na Frenk Mtasimwa (25, Mure Julius(26), Omary Charles(28) na Legnard Mwampete(30) ambapo baada ya kukamatwa upelelezi unaendelea.

Amesema kufuatia utambuzi wa askari hao, askari kumi walikamatwa lakini upelelezi umebaini kuwa askari wane ndiyo waliohusika na tukio hilo la mauaji hivyo jeshi la polisi limewafikisha jana katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Mbeya na kusomewa mashitaka na mwanasheria wa SerikaliAchiles Paul Mulisa.

Askari waliofikishwa mahakamani na kusomewa shitaka hilo ni pamoa na MT 101269 Omary Mwichande(24), MT 101271 Rajabu Mussa(23), MT 101263 Mussa Vuai Hassan (24) na MT 99506 Richard Costa Frisch(24) ambapo nwote wamekana shitaka lao na kesi imehairishwa mpaka Desemba 12, mwaka huu.

Kamanda Diwan Athuman ametoa wito kwa jamii kuepukana na tabia ya kujichukulia sheria mkononi na pindi wanapotendewa isivyo halali ni vizuri kutoa malalamiko yao katika mamlaka husika vilevile alisema kuwa ni vema jamii ikajenga tabia ya kutii sheria bila shuruti.

No comments:

Post a Comment