Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, December 20, 2012

Waasi wadhibiti mji wa mpakani Afrika ya Kati


Waasi wadhibiti mji wa mpakani Afrika ya Kati
Waasi nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati wameudhibiti mji wa kaskazini wa Kabo ulioko karibu na mpaka wa nchi jirani ya Chad. Afisa mmoja wa jeshi la Jamhuri ya Afrika ya Kati ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema waasi hao wa muungano wa Seleka wamekata mawasiliano yote na mji wa Kabo ambao wanaushikilia hivi sasa. Shambulio hilo la waasi limefanywa siku moja baada ya vikosi vya jeshi la Chad kuingia katika ardhi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati kuitikia ombi la serikali ya Bangui la kuisaidia kuzima uasi nchini humo. Wakati huohuo Umoja wa Afrika umewataka waasi wa Seleka kuondoka katika mji huo wanaoushikilia huku waasi hao wakisisitiza kusonga mbele kuelekea kusini mwa nchi hiyo.
Kamanda wa waasi hao Djouma Narkoyo amethibitisha kwamba wameuteka mji wa Kabo na wanasonga mbele kuelekea mji wa Batangafo. Waasi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati wametishia kumuangusha Rais wa nchi hiyo Francois Bozize aliyetwaa madaraka mwaka 2003 kupitia mapinduzi ya kijeshi. Waasi hao wanamtuhumu kiongozi huyo kuwa amekiuka makubaliano ya amani aliyofikia na makundiu tofauti ya waasi kati ya mwaka 2007 na 2011…/

No comments:

Post a Comment