Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, December 26, 2012

Asilimia 63.8 ya Wamisri waunga mkono katiba mpya


Asilimia 63.8 ya Wamisri waunga mkono katiba mpya
Jumla ya asilimia 63.8 ya Wamisri waliopiga kura katika kura ya maoni ya hivi karibuni nchini humo wameunga mkono kuidhinishwa rasimu ya katiba mpya ya nchi hiyo. Samir Abu al Matti Mkuu wa Kamisheni Kuu ya Uchaguzi ya Misri ametangaza matokeo hayo jana katika mkutano na vyombo vya habari huko Cairo mji mkuu wa nchi hiyo. Wakati huo huo Hisham Qandil Waziri Mkuu wa Misri ametoa taarifa akisema kuwa hakuna aliyeshindwa kwenye kura hiyo ya maoni na kwamba katiba mpya ya Misri itakuwa ya Wamisri wote. Ameyataka pia makundi yote ya kisiasa kushirikiana na serikali ili kuisaidia nchi hiyo kufufua uchumi wake. 

No comments:

Post a Comment