Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, December 5, 2012

Serikali ya Mali na waasi wafikia makubaliano



Serikali ya Mali na waasi wafikia makubaliano Serikali ya Mali na makundi mawili ya waasi yaliyodhibiti eneo la kaskazini mwa nchi hiyo mwezi Aprili mwaka huu yamekutana kwa mara ya kwanza na kukubaliana kufanya mazungumzo ili kuhitimisha mgogoro nchini humo. Hayo yameelezwa na waziri kutoka nchi mpatanishi Burkina-Faso.
Ujumbe wa serikali ya Mali jana ulikutana na wawakilishi wa kundi la kabila la Tuareg linalopigania kujitenga huko kaskazini mwa Mali ambalo uasi wake wa awali ulitekwa nyara na kundi la Ansaruddin lenye mfungamano na mtandao wa al Qaida. Kundi hilo la Ansaruddin liliwakilishwa pia na wajumbe wake katika mkutano wa Ouagadougou mji mkuu wa Burkina-Faso.  
Djibril Bassole Waziri wa Mambo ya Nje wa Burkina-Faso amesema kuwa jumbe hizo tatu zimekubaliana kwamba kuna haja ya kuanzishwa fremu ya mazungumzo ya kitaifa ya Mali kwa kuwashirikisha wawakilishi wa jamii mbalimbali zinazoishi huko kaskazini mwa Mali. Pande hizo tatu zimesema baada ya kumaliza mkutano wao kuwa zimekubaliana kumaliza uhasama kati yao.

No comments:

Post a Comment