Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, December 26, 2012

Kiongozi wa upinzani Zambia akamatwa na kuachiliwa


Kiongozi wa upinzani Zambia akamatwa na kuachiliwaKiongozi wa upinzani Zambia Nevers Mumba amekamatwa leo Jumatano na vikosi vya usalama na kuachiliwa baada ya kusailiwa.
Hii ni mara ya pili kwa Mumba kukamatwa katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita kwa tuhuma ya kuitisha mkutano wa hadhara bila kibali.
Mumba ambaye zamani alikuwa mwanachama wa chama tawala cha MDC sasa yuko katika chama kikuu cha upinzani cha MMD na katika siku za hivi karibuni ameongoza maandamano dhidi ya serikali ya Rais Michael Sata.
Wanasiasa wa upinzani wanamtuhumu Rais Sata kuwa anawakandamiza wapinzani. Serikali ya Zambia imekataa kuwapatia wapinzani vibali vya maandamano katika mji mkuu Lusaka.
Alipochaguliwa mwaka jana, Rais Sata aliahidi kupambana na ubadhirifu wa fedha za uma na kubuni nafasi za ajira. Wapizani wanadai serikali imeshindwa kutekeleza ahadi hizo.

No comments:

Post a Comment