Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, December 7, 2012

Pentagon yakiri ndege iliyonaswa Iran ni ya USA

Pentagon yakiri ndege iliyonaswa Iran ni ya USA
George Little Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) amekiri kwamba ndege isiyo na rubani iliyonaswa na Iran baada ya kuingia kinyemela katika anga ya Ghuba ya Uajemi imetengenezwa Marekani. Hata hivyo Little amedai kwamba kukamatwa ndege hiyo hakuthibitishi kwamba imetumwa nchini Iran na Marekani. Matamshi hayo ya msemaji wa Pentagoni
ni ya kwanza kutolewa na maafisa wa Marekani kuhusiana na ndege yao hiyo isiyo na rubani, suala ambalo wamekuwa wakilikana tangu habari hiyo ilipotangazwa na Iran. Jumatano Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) alitangaza kwamba wamefanikiwa kukamata ndege ya kijasusi ya Marekani isiyo na rubani punde baada ya kuingia katika anga ya Iran kinyume cha sheria. Aidha Brigedia Jenerali Ramazan Sharif  Mkuu wa Idara ya Habari ya IRGC alitangaza kwamba wamefanikiwa kuchomoa habari na taarifa zote za siri katika ndege hiyo ya kijasusi isiyo na rubani (drone) ya Marekani aina ya ScanEagle iliyonaswa hivi karibuni na jeshi la Iran.

No comments:

Post a Comment