Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, December 11, 2012

Ehsanoghlo: Hali ya Syria ni nyeti zaidi Ma/ Kati


Ehsanoghlo: Hali ya Syria ni nyeti zaidi Ma/ KatiKatibu Mkuu wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Nchi za Kiislamu OIC amesema kuwa hali ya mambo huko Syria ni nyeti. Ikmaluddin Ehsanoghlo amesema kuwa Syria iko katika mazingira nyeti zaidi na kwamba katika mazingira hayo nchi hiyo inapasa kujiepusha na mambo yasiyo na taathira yoyote katika kufanikisha kufikiwa mwenendo wa uhuru na demokrasia nchini humo. Katibu Mkuu wa Jumuiya ya OIC kesho Jumatano anatazamia kuelekea Morocco kwa ajili ya kushiriki kwenye kikao cha "Marafiki wa Syria." Syria imekuwa ikikabiliwa na hali ya mchafukoge tangu mwezi Machi mwaka jana, machafuko ambayo hadi sasa yamepelekea kuuawa wananchi vikiwemo vikosi vya usalama vya nchi hiyo. 

No comments:

Post a Comment