Duru za habari kutoka nchini Kodivaa
 zinaarifu kuwa, watu wasiojulikana wenye silaha wamekishambulia kituo 
cha upekuzi nchini humo na kuwajeruhi askari wawili. Watu walioshuhudia 
wamesema kuwa, askari walilazimika kujibu na hivyo kusababisha kuzuka 
mapigano kati ya vikosi vya usalama na watu hao wenye silaha. Tangu 
mwezi Agost mwaka huu Ivory Coast imekuwa ikishuhudia silsila ya mauaji 
ya kuvizia, yanayofanywa na watu wasiojulikana wenye silaha, 
dhidi ya 
askari wa kulinda usalama na vituo vya kijeshi nchini humo. Serikali ya 
Ivory Coast inayahusisha mauaji hayo na askari watiifu kwa aliyekuwa 
rais wa nchi hiyo Laurent Gbagbo, ambaye hivi sasa kesi yake inaendelea 
kusikilizwa na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC ya mjini Hague, 
Uholanzi. Hayo yanajiri katika hali ambayo, jana Mahakama Kuu ya Ivory 
Coast ilitangaza kukubaliana na ombi la aliyekuwa Waziri Mkuu wa Gbagbo 
Bwana Gilbert Marie Aké N'Gbo pamoja na watu saba wengine waliokuwa 
wapambe wa rais huyo, aliyetaka kuachiliwa huru kwa muda na mahakama 
hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment