Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, December 21, 2012

Watu wenye silaha wawashambulia askari Kodivaa


Watu wenye silaha wawashambulia askari Kodivaa
Duru za habari kutoka nchini Kodivaa zinaarifu kuwa, watu wasiojulikana wenye silaha wamekishambulia kituo cha upekuzi nchini humo na kuwajeruhi askari wawili. Watu walioshuhudia wamesema kuwa, askari walilazimika kujibu na hivyo kusababisha kuzuka mapigano kati ya vikosi vya usalama na watu hao wenye silaha. Tangu mwezi Agost mwaka huu Ivory Coast imekuwa ikishuhudia silsila ya mauaji ya kuvizia, yanayofanywa na watu wasiojulikana wenye silaha,
dhidi ya askari wa kulinda usalama na vituo vya kijeshi nchini humo. Serikali ya Ivory Coast inayahusisha mauaji hayo na askari watiifu kwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Laurent Gbagbo, ambaye hivi sasa kesi yake inaendelea kusikilizwa na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC ya mjini Hague, Uholanzi. Hayo yanajiri katika hali ambayo, jana Mahakama Kuu ya Ivory Coast ilitangaza kukubaliana na ombi la aliyekuwa Waziri Mkuu wa Gbagbo Bwana Gilbert Marie Aké N'Gbo pamoja na watu saba wengine waliokuwa wapambe wa rais huyo, aliyetaka kuachiliwa huru kwa muda na mahakama hiyo.

No comments:

Post a Comment