Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, December 4, 2012

Waasi wa M23: Tukipuuzwa tutarejea tena Goma


Waasi wa M23: Tukipuuzwa tutarejea tena Goma Waasi wa M23 wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wametishia kuwa watarejea tena katika mji wa Goma wa mashariki mwa nchi hiyo endapo serikali ya Kinshasa haitoafiki kufanya nao mazungumzo hadi kufikia Jumatatu ya leo.  Bertrand Bisimwa mmoja wa wasemaji wa M23 amesema kwamba, wanaumia sana kuondoka Goma hasa kutokana na kupoteza watu wao katika mapigano ya kudhibiti mji huo; lakini kwamba kama kufanya hivyo kutakuwa ni kutoa zawadi kwa mchakato wa amani wanalikubali hilo. Ameongeza kuwa, marafiki wa Kongo wamewashauri watoe fursa kwa mazungumzo; lakini kama mazungumzo hayo hayataanza hadi kufikia mchana wa leo, basi watarejea tena katika mji wa Goma. Hayo yanaripotiwa katika hali ambayo, tangu waasi wa M23 waondoke Goma, Rais Joseph Kabila hajaweka wazi hadi sasa kama serikali yake iko tayari kufanya mazungumzo na waasi hao.

No comments:

Post a Comment