Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, December 13, 2012

Milioni mia tatu wanakosa maji ya kunywa Afrika


Milioni mia tatu wanakosa maji ya kunywa Afrika
Idrissa Doucoure Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Kimataifa ya Maji na Afya ya Afrika amesema kuwa, watu milioni mia tatu wamekosa maji salama ya kunywa barani humo. Akihutubia kwenye kongamano la pili la taasisi hiyo huko Dakkar mji mkuu wa Senegal, Doucoure ameongeza kuwa, licha ya watu milioni mia tatu kukosa maji salama ya kunywa, wengine milioni mia tano wanakabiliwa na hali mbaya ya ukosefu wa huduma za afya. Kongamano hilo la siku mbili linawashirikisha wajumbe 700 wakiwemo mawaziri kutoka nchi 36 za Kiafrika linafanyika kwa shabaha ya kutafuta njia za kuwekeza katika sekta za maji na huduma za afya barani Afrika.

No comments:

Post a Comment