Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, December 5, 2012

Magaidi wa Syria wabomoa maduka Aleppo



Magaidi wa Syria wabomoa maduka Aleppo  Picha zilizochukuliwa kutoka katika mji wa Aleppo huko kaskazini magharibi mwa Syria zinaonyesha wamiliki wa maduka mjini humo wakiuza bidhaa zao mitaani kufuatia kubomolewa maduka yao na makundi ya magaidi na waasi wanaopigana dhidi ya serikali ya Rais Bashar al Assad wa nchi hiyo.
Makundi hayo ya wahalifu wenye silaha ambao wengi wao ni raia wa kigeni wamebomoa na kuiba bidhaa zilizokuwa ndani ya maduka hayo. Ripoti zinasema kuwa magaidi hao wanaiba pia ngano na kuiuza nchini Syria. Septemba 29 mwaka huu moto mkubwa uliharibu mamia ya maduka katika mji huo mkongwe uliotangazwa na Unesco kuwa ni eneo la turathi za kimataifa. Moto huo ulizuka wakati kulipozuka mapigano makali kati ya waasi na vikosi vya serikali.

No comments:

Post a Comment