skip to main |
skip to sidebar
Wapinzani Kongo wataka kukomeshwa mapigano
Wapinzani nchini Kongo wametaka kukomeshwa vita huko mashariki
mwa nchi hiyo kufuatia kuendelea mapigano katika mkoa wa Kivu ya
Kaskazini. Lucien Mbusa Katibu Mkuu wa Harakati ya Ukombozi wa Kongo
amesisitiza kwamba wapinzani nchini Kongo wanataraji kuwa Ufaransa
itatumia ushawishi ilionao katika taasisi za kimataifa na hivyo kufanya
juhudi za kumaliza mapigano mashariki mwa nchi Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Kongo. Lucien Mbusa ambaye ni mjumbe wa wapinzani katika bunge la
Kongo
amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Francois Hollande wa
Ufaransa mwishoni mwa kikao cha Francophone mjini Kinshasa.
Katibu Mkuu wa Harakati ya Ukombozi wa Kongo amesifu matamshi ya Rais
wa Ufaransa kuwa matokeo ya uchaguzi wa Rais wa nchi hiyo ni yenye
kutia shaka, kwamba kuna ukiukaji wa haki za binadamu na pia raia wa
Kongo wanafungwa jela bila ya kuhukumiwa.
No comments:
Post a Comment